Wednesday 24 August 2016

Lady Jaydee: Fahamu muziki anaosikiliza, simu anayotumia na app anayoipenda

Lady Jaydee ni shabiki pia wa muziki wa wasanii wengine.
13732334_1765420870367468_1104627438_n
Akihojiwa na jarida la The Africa Report, Jaydee alieleza kuwa pale anapokuwa amekwama kwenye foleni, husikiliza nyimbo za wasanii kama Bruno Mars, Whitney Houston pamoja na muziki unaochezwa kwenye vituo vya redio.
“Lakini nasikiliza aina mbalimbali ya muziki, hip hop, rnb, Jazz, afropop, muziki wa asili wa Tanzania, sina aina moja ya muziki wa kusikiliza,” alisema.
14052446_1119883834767634_1195663385_n
Kuhusu simu anayotumia, Jide alisema anapenda iPhone 6s yake na kwamba app anayoipenda ni Beauty Plus anayodai huchukua picha vizuri na uwezo wa kuzitengeneza vyema.

No comments:

THIS BLOG DESIGNED BY

HOME BOYZ GRAPHICS LABORATORY