Thursday 4 January 2018

Maneno ya Ridhiwan Kikwete baada kuiona video ya Fresh Remix, adai Fid Q katii kauli ya Rais


December 12, 2017 President  Magufuli aliwataka Jumuiya ya Wazazi ya CCM kutokaa kimya  wanapoona mambo mabaya katika jamii na akasema kuwa amekuwa akikerwa na tabia ya baadhi ya wanawake kwenye video za wasanii wa bongo kuvaa vibaya na kuonyesha maumbile yao. ya ndani.
Leo January 4, 2018 Mbunge wa Chalinze (CCM) Ridhiwani Kikwete amempongeza Fid Q baada ya kuonesha kutii kauli ya JPM ambayo aliitoa kwenye Kamati Kuu ya CCM.
Ridhiwani ametoa pongezi hizo kupitia account yake ya Twitter baada ya kuiona video mpya ya Fid Q  aliyomshirikisha Diamond Platnumz na Rayvanny  ‘Fresh Remix’ ambapo ndani Video Queens wameonekana kuvaa magauni marefu ambayo yamewasitiri.
“Hii inaitwa tii bila shuruti. Hongera sana mdogo wangu Diamond, Fid Q kwa kuonyesha usikivu. Mavazi mazuri ni yale yanayohifadhi utu na jinsi. Mtoto umleavyo ndivyo akuavyo” – Ridhiwani Kikwete

Hii inaitwa Tii Bila Shuruti. Hongera sana Mdogo wangu @diamondplatnumz , @FidQ kwa kuonyesha usikivu. Mavazi Mazuri ni Yale yanayohifadhi Utu na Jinsi. 

No comments:

THIS BLOG DESIGNED BY

HOME BOYZ GRAPHICS LABORATORY